DKT. MOLLEL AWATAKA WANANNCHI KUTOFICHA WATOTO WENYE USONJI
Author -
MUUNGANO MEDIA
Jumapili, Desemba 03, 2023
0
NAIBU Waziri
wa Afya Dkt. Godwin Mollel ametoa wito kwa wananchi kutowaficha watoto
wenye changamoto ya Usonji (autism) kwani wakipata malezi na mafunzo
mazuri watasaidia kuleta matokeo chanya katika jamii.
Dkt. Mollel
amesema hayo leo Desemba 3, 2023 wakati akifungua Mkutano wa kimataifa
wa Usonji (autism) uliofanyika katika kituo cha kimataifa wa Julius
Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Ikumbukwe kuwa Usonji ni tatizo
linalojitokeza mapema utotoni, ambapo mtoto huwa na mapungufu kwa
kupenda kujitenga na kutotaka kuwa karibu na watu (Impaired social
interaction), hupata matatizo ya lugha na shida ya mawasiliano (impaired
language and communication skills) na huwa na tabia ya kurudia rudia
kitu anachokifanya mara nyingi (restrictive repetitive behaviour).
Mara
nyingi wazazi hugundua watoto wao wana tatizo hili katika kipindi cha
miaka miwili ya umri wa mtoto.Chanzo halisi cha tatizo hili la usonji
hakijulikani ingawa matatizo ya kijenetiki (Neurodevelopmental disorder)
ndio uhusishwa na tatizo la usonji.Maaambukizi ya Rubella au matumizi
ya pombe na madawa ya kulevya aina ya coccaine wakati wa ujauzito na
hata sababu za kimazingira, yote haya uhusishwa na tatizo hili la
usonji.