TUME YA HAKI ZA BINADAMU KUANZA UCHUNGUZI KIFO CHA MWANAFUNZI UDOM.

MUUNGANO   MEDIA
0

 


Na. Gideon Gregory, Dodoma.

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora  (THBUB) Jaji mstaafu Mathew Mwaimu amesema kuwa Tume hiyo inaanza kufanya uchunguzi juu ya kifo cha Bi. Nusura Hassan Abdallah, aliyekuwa mwanafunzi wa chou kikuu cha Dodoma (UDOM), shahada ya kwanza ya sanaa katika Elimu (BA.Ed) katika Ndaki ya Insia ya sayansi ya chou hicho kilichotokea wiki mbili zilizo pita.

Jaji mstaafu Mwaimu ameyasema hayo leo Mei 10,2023 Jijini Dodoma wakati akizungumza na vyombo vya Habari na kubainisha kua uchunguzi huo utaanza mara moja ambapo kwasasa mchakato bado unaendelea na mara watakapo maliza uchunguzi huo watatoa taarifa juu ya kile kilichotokea.

Amesema lengo la kufanya uchunguzi huo ni kupata ukweli kuhusiana na tukio hilo na kuondoa mkanganyiko uliopo na maneno kuwa mengi.

“Tume imeona taarifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari hususani mitandao ya kijamii kuhusu kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma Bi Nusura Hassan Abdallah aliyekuwa mwananfunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho. Kwa mujibu wa taarifa, imedaiwa kuwa Bi Nusura Hassan Abdallah alifariki katika hospitali ya Faraja, huko Himo mkoani Kilimanjaro, kwa hali yoyote ile taarifa za kifo cha mwanafunzi huyo ni za kusikitisha kwa kuwa kifo hicho, iwe kwa sababu yoyote ile, kimekatisha ndoto ya maisha yake na haki yake ya kupata elimu ya juu,”amesema.

Amesema Tume hiyo inatambua kuhusu kuwepo kwa vyombo vinavyoshughulikia masuala ya haki jinai hususani Jeshi la Polisi na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambapo katika mazingira ya kawaida vyombo hivyo vinahusika kulishughulikia suala hilo na wanatambua hilo na tume inavipa heshma vyombo hivyo katika utekelezaji wa majukumu yake na kazi kubwa ambayo vinafanya.

Hata hivyo, kunapotokea mashaka kutoka kwa wananchi kuhusu jambo lolote linaloashiria uvunjwaji wa haki za binadamu au mashaka ya haki kutokutendeka, Tume inayo mamlaka ya kufanya uchunguzi juu ya jambo hilo kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya Tume kwa kuwa inalo jukumu la kutetea na kulinda haki za binadamu nchini,”amesema.

Aidha, ameongeza kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Sura ya 391 Tumehiyo ina mamlaka ya kuanzisha uchunguzi wake yenyewe juu ya malalamiko yanayoashiria uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora pasipo kusubiri kuletewa malalamiko.

Kwa muktadha huo Tume imeazimia kufanya uchunguzi wake huru kwa madhumuni ya kubaini ukweli kuhusu matukio hilo,”ameongeza.

Amesema Tume hiyo inachunguza mambo mengi sio tu, tukio hilo bali imekuwa ikichunguza matukio na matukio mengine yanayokiuka misingi ya haki za binadamu.

Ikumbukwe kuwa kifo cha Nusura Hassan Abdallah kilidhibitishwa na kitengo cha masoko na mawasiliano cha Chuo Kikuu Dodoma (UDOM), Mei 5,2023 baada ya kupokea taarifa kutoka kwa mwanafunzi ambaye alikuwa anasoma naye kuwa amepokea taarifa kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa mjomba wake marehemu ikimjulisha kuwa Nusura amefariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitari ya Faraja iliyopo Himo, Kilimanjaro.

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)