RC CHALAMILA AIPONGEZA TIMU YA WATALAAM WA AFYA KWA KUJIDHATITI KUELIMISHA JAMII KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MARBURG.

0

Albert  Chalamila Mkuu wa Mkoa wa Kagera akizungumza katika kikao cha kamati  ya Wajumbe Maalum  wa kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg  kilichofanyika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Dkt.Issesanda Kaniki Mganga Mkuu Mkoa wa Kagera akizungumza katika kikao cha kamati  ya Wajumbe Maalum  wa kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg  kilichofanyika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

 


 



Wajumbe Maalum  wa kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg  kilichofanyika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.
 

 

Na.Elimu ya Afya kwa Umma.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe.Albert Chalamila ameipongeza Timu ya Watalaam wa Afya kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu,  Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais TAMISEMI, ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wanawake na Makundi Maalum ,Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa pamoja na wadau kutoka mashirika mbalimbali ya Kitaifa na  Kimataifa kwa kuendelea kushirikiana na Mkoa katika Mapambano ya Ugonjwa wa Marburg.

Mhe.Chalamila ametoa pongezi hizo leo April, 10, 2023 katika kikao cha kamati  ya Wajumbe Maalum  wa kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg  kilichofanyika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Mhe.Chalamila amesema kazi inayofanywa na kamati hiyo ni kubwa sana katika kukabiliana na ugonjwa wa Marburg .

“ Nitumie nafasi hii kuwapongeza kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya, na ninyi kutoka mashirika ya Kimataifa mmetusaidia sana kufikisha ujumbe uliosahihi  na taswira ya nchi yetu kwa mataifa mbalimbali na ninachosisitiza ninyi wataalam wa afya lazima muwe na ujasiri wa kitaaluma”amesema.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera Dkt.Issesanda Kaniki ametoa shukrani na pongezi kwa Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu  kwa kuchukua hatua za haraka  ikiwemo kutuma timu ya madaktari bingwa 12 wameweka kambi mkoani Kagera mara tu ugonjwa wa Marburg uliporipotiwa.

“ Kama tunavyofahamu ugonjwa huu unakimbilia kwenye viungo muhimu kama figo kutofanya kazi, tulikumbana na changamoto ambapo ilibidi tuwe na madaktari bingwa kwa jitihada za Mkoa kwa kushirikiana na Waziri wa  Afya tuliweza kupata madaktari bingwa 12”amesema.

Aidha, Dkt. Kaniki amesema jumla ya watu  212 waliotangamana na wagonjwa wamefuatiliwa  ,kati yao   watu 174 wamekamilisha siku 21 za uangalizi hadi kufikia April, 8,2023.

 

Mkurugenzi Msaidizi  Sehemu ya  Epidemiolojia na udhibiti wa Magonjwa kutoka Wizara ya Afya   Dkt. Vida Mmbaga amesema wanafanya mahojiano na watu mbalimbali ikiwemo watu mashuhuri  kwa ajili ya kufanikisha kupata taarifa kwa kuwepo kwa mgonjwa katika maeneo husika.

MWISHO

 

 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)