ZAIDI YA TSH.BILIONI 3 KUTOLEWA NA MAREKANI KWA AJILI YA KUKABILIANA NA MARBURG TANZANIA.

0

 


                       


Serikali ya Marekani   kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) lina mpango wa kutoa Dola za Kimarekani  milioni 3. Sawa na Tsh.Bilioni 3 katika shughuli za kujikinga na matibabu katika kukabiliana na ugonjwa wa Marburg ulioripotiwa hivi Karibuni Mkoani Kagera.

Fedha hizo zitasimamiwa na Shirika la Afya Duniani(WHO) pamoja na Shirika la kuhudumia Watoto Duniani(UNICEF).


Hayo yamejiri baada ya ujio wa ziara ya Makamu wa Rais nchini Marekani  Mhe.Kamala Harris ambapo pia amesema serikali yake kupitia Kituo cha Udhibiti wa Maradhi(CDC) inashirikiana na Tanzania  katika ngazi zote ikiwemo msaada  wa kitaalam katika kukabiliana  na mlipuko wa Virusi vya Marburg.

Aidha, Mhe.Kamala amesema Serikali ya Marekani itaendelea kuweka jitihada za pamoja na serikali ya Tanzania  katika utoaji wa elimu ya  afya pamoja na msaada wa vifaa tiba na mavazi ya kujikinga (Personal Protective Equipment) katika kuwasaidia Wahudumu wa Afya hapa nchini wanaopambana na mlipuko wa Marburg.

Kwa upande wake Rais wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ameishukuru Serikali ya Marekani kwa kuendelea kuwa na Ushirikiano  na  kubainisha kuwa nia ya Tanzania ni kuendelea kuwa na ushirikiano mwema katika nyanja mbalimbali.

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni serikali ya Tanzania ilithibitisha watu watano kati ya wanane kufariki dunia kutokana na ugonjwa wa virusi vya homa ya Marburg katika mkoa wa Kagera, Kaskazini Magharibi mwa nchi hii..

 


Hata hivyo Waziri wa Afya , Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari   Machi 21, 2023 jijini Dar es Salaam alisema Serikali imefanikiwa kuuzuia ugonjwa huo kutoka nje ya mipaka ya mkoa wa Kagera.

 

Ugonjwa huo unaoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine au kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu unatajwa kutokuwa na tiba bali hutibiwa kwa dalili husika anazokuwa nazo mtu.

 


Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)