WITO WATOLEWA KWA WASHIRIKI KUONGEZA JUHUDI KUUOMBEA ULIMWENGU HASA KATIKA HIZI SIKU ZA MWISHO

0

 

 


Na.Faustine Gimu Galafoni

Katika kuadhimisha siku ya wanawake wa Kiadventista  ya Maombi Duniani,Washiriki wa kanisa la Waadventista Wasabato wameaswa kuongeza juhudi  kufanya maombi kwa ajili ya kuiombea dunia hasa katika kipindi hiki kigumu cha  siku za mwisho zilizojaa wasiwasi,maasi na vita.

Hayo yalibainishwa  Mwishoni mwa Juma lililopita  na  baadhi ya akina mama kutoka kanisa la Waadventista Wasabato  Chang’ombe  Dodoma  wakati wakifanya mahojiano maalum na  mtandao huu  mara baada ya kufanyika ibaada ya Sabato kanisani hapo.

 

 

Beth Swai,mkurugenzi idara ya wana wa kike Kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe Cecilia Kisaka ,pamoja na Haika Joas ni miongoni mwa wanawake na washiriki wa kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe  walisema katika kuadhimisha siku ya maombi kwa wana wa kike ,kwa kumtazama Nabii Yoshua kama mtumishi wa mungu ,mcheshi ,msafi na mwenye ucha Mungu inapaswa kila mkristo kuwa na upatanisho katika maombi.

 

“Tumeona Yoshua alivyosimama katika maombi hakutetereka hivyo na sisi kama washiriki tunapaswa kusimama imara katika maombi,hivyo katika maombi hakuna kuchoka  ni wakati wa kusonga mbele”alisema mmoja wa akina mama hao.

Aidha,mkurugenzi idara ya wana wa kike Kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe  Dodoma Cecilia Kisaka alisema katika kuadhimisha siku ya maombi ya kimataifa ya wana wa kike waliandaa program mbalimbali katika kanisa hilo zikiwemo programu za mahubiri,pamoja na ibaada za nyimbo kwa wanawake.

 

 

 

 

Akihubiri katika siku ya kimataifa ya wanawake  ya maombi kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe mkurugenzi idara ya watoto kanisani hapo Jackline Masikini  amekazia  kwa kila mwumini kuwa karibu na uhusiano na Mungu.

Akibainisha kupitia somo lililokwenda na kichwa kisemacho”Kuomba katika siku za mwisho  Cecilia alisema mwanadamu anaweza kuzungumza na Mungu endapo ataweka mahitaji yake na maombi hutunza kumbukumbu  huku akinukuu kitabu cha Yoshua 5:13  jinsi Yoshua  alipokuwa karibu na mji wa Yeriko na alivyokuwa jasiri katika maombi na kukabiliana na changamoto zilizomkabili.

Sisi sote tunatakiwa kuwa  karibu na Mungu kwa njia ya maombi kwani tutakuza uhusiano wetu na mungu,tutaondoa hofu zinazotawala hasa katika maisha yetu ya leo, na kukuza kumbukumbu zetu kupitia maombi,kwani yanaweza hata kubadili na kurahishisha hata jambo lisilowezekana”alisema.

 


 


Mkurugenzi idara ya watoto kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe  Jackline Masikini akitoa huduma ya mahubiri katika siku ya kimataifa ya wanawake ya maombi kwa kanisa la Waadventista Wasabato Ulimwenguni.

 

Akitoa neno katika ibaada ya watoto kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe , ELLEN  LUPIA aliwaasa watoto kuwa watii kwa  wazazi wao na kuhakikisha wanaenda katika mienendo mizuri kwani inaepusha wizi na vifungo visivyo vya lazima.

“Watoto tunapaswa kuwa na tabia njema ,mnajua wizi ni mbaya ,hivyo mara nyingi mtoto anayekuwa na tabia mbovu ni yule asiyekuwa na utii kwa wazazi na tabia ya udokozi huanza polepole “alisema.


 


Ellen  Lupia akihubiri katika ibaada ya watoto katika kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe jijini Dodoma .

MWISHO.

 

 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)