PROF. NDALICHAKO APIGA MARUFUKU WAKUU WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA KUWAWEKA NDANI[KORTINI] WATUMISHI WA UMMA KWA MAKOSA YASIYO YA JINAI.

0

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI


 

 


Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu[Kazi ajira,vijana ,na wenye ulemavu]Prof.Joyce Ndalichako.


Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

 

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu[Kazi ajira,vijana ,na wenye ulemavu]Prof.Joyce Ndalichako amepiga marufuku kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya  nchini tabia ya kuwaweka ndani[kortini] watumishi wa umma wenye makosa yasiyo ya jinai.

Prof.Ndalichako amepiga marufuku hiyo leo Machi 12,2022 jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa  baraza kuu  la  shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania[TUCTA]  ambapo amesema haipaswi kuwekwa ndani watumishi wa umma kwa makossa yasiyo ya jinai kwani pamekuwa na tabia ya wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kuwaweka ndani watumishi wa umma kwa makossa yasiyo ya jinai.



Baadhi ya wanawake kamati ya wanawake shirikikisho la vyama wafanyakazi[TUCTA]wakimpokea kwa  shangwe ,Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu[Kazi ajira,vijana ,na wenye ulemavu]Prof.Joyce Ndalichako  .  


Hivyo,amesema makosa ya kiutendaji kwa watumishi yachukuliwe hatua sehemu za kazi.

"Hilo suala la kuwaweka ndani watumishi kwa makosa yasiyo ya jinai ,niendelee kuwakubusha waendelee kufuata miongozo iliyowekwa "amesema.

Aidha,Prof.Ndalichako amewaagiza waajiri wote nchini kuhakikisha vikao vya mabaraza ya wafanyakazi vifanyike kwa mujibu wa matakwa ya kisheria ikiwemo kulipa posho stahiki kwa wafanyakazi.

"Nichukue nafasi hii kuyaagiza mabaraza ya wafanyakazi yafanyike kwa mujibu wa sheria"amesema.

Rais wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania[TUCTA]  Tumaini Nyamhokya  amesema  kuna haja kwa serikali kutekeleza  ipasavyo kuwarejesha kazini watumishi wa darasa la saba kwani kuna baadhi ya taasisi zimekuwa zikiwakataa na kuwanyima stahiki zao .


Baadhi ya washiriki mkutano wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi[TUCTA]wakifuatilia wakifuatilia mada zilizokuwa zinatolewa katika mkutano huo jijini Dodoma.


"Kama alivyosema Rais ,suala la kuwarejesha kazini wa darasa la saba ,nalo linapaswa kuangaliwa upya kwa sababu sio makosa yao"alisisitiza.



Rais wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania[TUCTA]  Tumaini Nyamhokya 

Mwenyekiti wa kamati ya wanawake wa shirikisho hilo Rehema Ludanga amesema  kuwa bado kuna changamoto ya utekelezaji wa sheria ya mkataba wa kazi.


Mwenyekiti wa kamati ya wanawake wa shirikisho hilo Rehema Ludanga.

"Changamoto kubwa tunazokabiliana nazo mpaka sasa hivi kuna  baadhi ya maeneo bado utekelezaji wa sheria hauko sawasawa "amesema. 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)