ZAIDI YA WATOTO 400 WAKAMATWA KAHAMA KWA KIPINDI CHA MWEZI JAUARI HADI DISEMBA WAKISAFIRISHWA KU

0
 Image result for ukatili wa watoto
  PICHA KUTOKA MAKTABA

Imeelezwa kuwa jumla ya watoto 400 katika halmashauri ya mji wa Kahama wamekamatwa wakisafirishwa ndani na nje ya nchi katika kipindi cha mwezi januari hadi desemba kwa lengo la kupelekwa kufanya kazi katika maeneo mbali mbali.

Hayo yamebainishwa katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyoadhimishwa katika bwalo la polisi mjini kahama.

Akisoma taarifa ya halmashauri afisa maendeleo ya jamii kutoka katika hamashauri ya mji wa Kahama  Marry Chima amesema kuwa jumla ya watoto 400 wamekamatwa wakisafirishwa kutoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi ambapo amesema watoto 360 ni kutoka nchini Burundi watoto 20 kutoka Rwanda na wengine 20 wakitoka chini hapa katika maeneo ya Ngara na Kigoma.

Ameongeza kuwa katika kuendelea kupambana na suala la ukatili wa kijinsia  nchini watoto 27 wamelazimika kukatisha masomo baada ya kubainika kuwa na ujauzito jambo ambalo linakatisha ndoto zao na  linapaswa kukemewa kwa nguvu zote.
Naye mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Kahama bw, Abel Shija ambaye alikuwa mgeni rasimi katika maadhimisho hayo amesema kuwa serikali kwa kushirikiana na taasisi mashirika na wadau mbalimbali wanapashwa kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii kwani ndio msingi utakaowezesha kutokomeza ukatili katika jamii.

Maadhimisho ya ukatili a kijinsia hufanyika kila mwaka ifikapo novemba 25 hadi disemba 10 ambapo leo kilele cha maadhimisho hayo yamefanyika katika ukumbi wa bwalo la polisi mjini kahama huku kauli mbiu isemayo ukatili dhidi ya wanawake na watoto hautomuacha mtu salama ,chukua hatua pinga ukatili.
mwisho

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)