KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU WA KRISMAS NA MWAKA MPYA MAJAMBAZI YAINGIA NA MBINU YA UOMBAJI WA PESA KWA LAZIMA SUNGAMILE KAHAMA

0

Image result for maua ya sikukuu

Katika kuelekea msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka,vitendo vya wizi katika kijiji cha sungamile halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Mkoani shinyanga vimeongezeka baada ya wahalifu kuanza kuvamia kaya hadi kaya pamoja na  maduka na kupora mali mbalimbali.

mwenyekiti wa kijiji cha Sungamile Ngusa Mayunga amesema kuwa matukio ya wizi katika kijiji hicho yamekithiri likiwemo na tukio la majambazi kutembea mtaa kwa mtaa na kuomba pesa kwa lazima huku wakitumia bunduki kwa kutishia.


Siku ya kwanza waliiba zaidi ya shilingi milioni moja na laki 7 ambapo walikuwa wanadai kwa nguvu.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa mara baada ya siku moja kupita duka moja mali ya Mfanyabiashara aliyejulikana kwa jina moja la Mashaka liliporwa vitu mbalimbali vikiwemo simu za mkononi 6,mafuta ya kupikia ,sukari  pamoja na vocha.
Katibu wa muda wa  wafanyabiashara wa kijiji hicho Nzego Mihambo ametaja thamani ya vitu vilivyoibiwa ambapo ni zaidi ya shilingi laki saba.

Nao wananchi wa kijiji cha sungamile wamezungumzia kutokana na vitendo vya uhalifu kukithiri kijijini hapo huku wakiiomba serikali kuimarisha ulinzi na usalama ili kutokomeza vitendo vya wizi.

Hivyo kutokana na tukio hilo la kuporwa duka  ambalo limetokea usiku wa kuamkia jana jeshi la jadi  sungusungu sungamile liliamuru mlinzi aliyekuwa katika zamu Shangalile Elisha  kulipa fidia zote bila kujali katiba ya umoja wa wafanyabiashara wa kijiji hicho ambapo inasema kuwa pindi panapotokea hitilafu wenye wajibu wa kulipa ni walinzi wote.
Na.Faustine Gimu Galafoni.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)