ELIMU BURE YAWA CHANGAMOTO YA MSONGAMANO WA WATOTO GEITA KWA KUKOSA VYUMBA VYA MADARASA

0


 Image result for MRUNDIKANO WA WANAFUNZI KWA KUKOSA VYUMBA VYA MADARASA

 PICHA:KUTOKA MAKTABA




Na.Shija Felician,Geita

Idadi kubwa ya wanafunzi katika shule ya msingi Kasandalala wilayani Mbogwe mkoani Geita wanasomea nje madirishani baada ya vyumba vya madarasa kujaa kutokana na msongamano mkubwa watoto waliotokana na mpango wa serikali wa elimu bure.

Hali hiyo imeelezwa jana  na mtendaji wa kijiji cha Shinyanga B kata ya Nyakafulu wilayani Mbogwe Machibya Elias wakati wa tathimini wa mradi wa utawala bora na uwajibikaji unaotekelezwa na shirika  Capacity Building Initiatives for poverty alleviation CABUIPA ambapo amesema hali hiyo imesababisha ufundishaji wa wanafunzi kuwa mgumu.

Elias amesema kutokana na msongamano huo wanafunzi wa darasa la pili wanaoingia la tatu wako mia saba na wale wa darasa la kwanza wanaoingia la pili wako mia tano na wote wameandikishwa kwenye mpango wa serikali wa elimu bure ambapo kila darasa wanasoma chumba kimoja na shule hiyo ina wanafunzi elfu tatu mia moja themanini huku ikiwa na vyumba saba tu vya madarasa.

Naye mwezeshaji wa utawala bora kutoka shirika la  Capacity Building Initiatives for poverty alleviation CABUIPA Michael Ikila amewataka viongozi wa serikali katika kijiji hicho kila mmoja kutumia wajibu wake kwenye madaraka aliyonayo kuonesha ushirikiano kumaliza tatizo hilo kutokana na maendeleo huletwa na wananchi wenyewe.

Kwa upande wake ofisa elimu wa wilaya ya Mbogwe Samwel Muyemba amesema tayari kuna mkakati wa kumaliza tatizo hilo shuleni hapo kwa kuigawa mara mbili shule hiyo pamoja na kupunguza wanafunzi kwa kuwapeleka shule jirani ingawa tayari kuna ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa ambayo yatakamilika kabla ya wanafunzi hawajafungua mwezi Januari.

Mwisho

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)