WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YAWAITA WATANZANIA KUFIKA 88 ILI KUPATA ELIMU YA KATIBA NA SHERIA.

MUUNGANO   MEDIA
0

 



Na Avelina Musa - Dodoma.


Kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika October mwaka huu Wizara ya Katiba na Sheria imewataka watanzania kufika katika Banda la Wizara hiyo  ili kupata elimu ya katiba na Sheria zote za Nchi.


Hayo yamesemwa Leo August mosi na Abdulrahman Msham, Mkurugenzi Msaidizi huduma za  Sheria kwa Umma kutoka wizara ya Katiba na Sheria katika  maonesho ya siku kuu ya wakulima Nane nane(8)ambayo kitaifa   yanafanyika Jijini Dodoma.


Amesema wizara hii imepewa idhini ya kusimamia masuala ya haki,Sheria na katiba ambapo watakapofika katika Banda hilo watapata elimu ya Sheria zote za nchi na watapata huduma mbalimbali.


Abduramani amesema kero nyingi wanazozipokea mara kwa mara ni  migogoro ya ardhi na migogoro ya mirathi pamoja na migogoro ya ndoa na talaka hasa katika mgawanyo wa mali baada ya ndoa na talaka.


"Sisi tupo hapa katika maonesho haya ambapo tunatoa huduma ya kutatua migogoro na  elimu ya utatuzi wa migogoro pamoja na elimu ya haki za binadamu."Amesema Abduraham.



"Na migogoro yote hii inatokana na watanzania kukosa elimu sahihi ya sheria ambapo ukosefu wa elimu ya Sheria inawafanya wanaingia katika migogoro isiyo ya lazima kama kutokuandika wosia."Amesema.


Maonesho ya sikukuu ya wakulima nane nane (88)yanafanyika kitaifa Jijini Dodoma kuanzia Leo August mosi Hadi August 8 mwaka huu ambayo yanaongozwa na kauli mbiu isemayo "Chagua viongozi Bora kwa maendeleo Endelevu ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi 2025".






Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)