CHUKUENI TAHADHARI DHIDI YA MAGONJWA YA MLIPUKO-DKT. SAMIA

MUUNGANO   MEDIA
0

 .


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mji mdogo wa  Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara baada ya kutokea maafa ya mafuriko.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mgonjwa katika Hospitali ya Wilaya Hanang(Tumaini) mkoani Manyara .

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa amembeba mmoja watoto walio katika kambi ya Waathirika wa Mafuriko Mji mdogo wa Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia baadhi ya wagonjwa na Waathirika wa Mafuriko katika moja ya Kambi Mji mdogo wa Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akielekea kuwajulia hali Wagonjwa wakiwemo majeruhi wa mvua ya mafuriko Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara.

 

Mtaa wa Katesh Sokoni Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara  ambapo soko lote lilifunikwa na tope lililochangamana na takataka mbalimbali  ambazo ni hatari kwa afya hivyo  kuwa na  uwezekano wa kupata Magonjwa ya mlipuko ikiwemo Kipindupindu.

Tahadhari za Kiafya zimekuwa zikitolewa ikiwemo wananchi kutoingia kwenye maji hayo bila kuvaa Kinga kwani ni hatari kiafya.

 

Wataalam kutoka Wizara ya Afya , Mratibu   Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii(CHWs )wa kijiji cha  Jorodom Kati wakitoa elimu ya kutumia vidonge vya kutibu maji na kutoa elimu ya Usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo. Elimu hii inatolewa nyumba kwa nyumba

 

 

Upatikanaji wa Maji safi na salama baada ya kuchimbwa visima virefu Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara itasaidia kuepukana na Magonjwa ya kuhara na kutapika.

 Uchimbaji wa Visima hivi umefuatia baada ya mifumo ya miundombinu ya maji kuharibiwa na mafuriko hivyo kusababisha kuchangamana na maji taka kutoka vyooni na Sehemu zingine zisizo salama kwa afya.

 Na.Elimu ya Afya kwa Umma.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi Mji mdogo wa Katesh Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuchukua tahadhari za magonjwa ya mlipuko kwa kuzingatia kanuni za afya ikiwemo matumizi ya maji safi na salama.

 

Dkt. Samia ametoa wito huo Disemba 7 ,2023 wakati akizungumza na wananchi  mji mdogo wa Katesh Wilayani Hanang Mkoa Manyara baada ya Disemba 3, 2023 kukumbwa na maafa ya mafuriko yaliyosababisha maporomoko ya udongo kutoka mlima Katesh na kusababisha madhara makubwa ikiwemo majeruhi,vifo na upotevu wa mali.

 

"Jambo kama hili linapotokea huwa yanatokea magonjwa ya mlipuko ,niwaombe wananchi wachukue hatua stahiki za kuzingatia kanuni za afya pindi wanapotumia maji wazingatie kuepuka magonjwa ya mlipuko ikiwemo kuhara "amesema.

 

Aidha, Rais Samia ametoa maagizo kwa Wizara ya Afya kuhakikisha elimu na ufuatiliaji kwa kina inatolewa kwa wananchi.

 

"Wizara ya Afya hakikisheni elimu juu ya kujikinga na madhara yanayoweza kutokea kutokana na mafuriko inatolewa pia kufuatilia kwa kina majeruhi mpaka kuhakikisha wanakuwa katika hali ya kawaida"amesema.

 

Halikadhalika, Dkt.Samia ameagiza kuhakikisha msaada wa Kisaiklojia unaendelea kutolewa pamoja na huduma za maji safi na salama kuendelea kuimarishwa.

 

Hata hivyo,ametumia fursa hiyo kuwashukuru wadau kwa kutoa msaada ambapo jumla ya Tsh.Bilioni 2.5 zimetolewa na wadau kutoka nje ya nchi huku akielekeza zitumike kujenga makazi ya kudumu kwa waathiriwa.



 

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)