WANAUME WASISITIZWA KUPIMA AFYA ZAO KWA HIARI.

MUUNGANO   MEDIA
0

 


Na Carlos Claudio, Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa msisitizo kwa wakina baba kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upimaji wa hiari wa Virusi Vya Ukimwi kuelekea maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani.

 

Mhe. Mhagama ameyasema hayo leo Novemba 14,2023 Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yatakayo fanyika kitaifa mkoani Morogoro Desemba 1 huku yakitanguliwa na wiki ya UKIMWI itakayozinduliwa Novemba 24 mwaka huu.

 

“Tunatumia maadhimisho haya katika kuhakikisha kwamba tunatoa taarifa za nchi zinazohusu udhibiti wa VVU na Ukimwi lakini pia katika maadhimisho haya na wiki nzima tunaitumia pia kutoa huduma za upimaji na hasa upimaji wa hiari wa VVU na hapa leo nimeanza kwa kuhamasisha tuanze kukumbuka kwamba ni wiki ambayo angalau kila mmoja kwa hiari yake anaweza kuitumia kama wiki ya kupima afya yake”.

 


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwera amesema kuwa wanaume wengi nchini hupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo kwakuwa hawana utamaduni wa kutambua hali zao.

 

“Kwenye tafiti zote wanaume wapo nyuma lakini pia hata ukiwa unaangalia takwimu ambazo zinaonysha matokeo ya tiba wanaume kwa ujumla ni wavivu sana kwenda kupata huduma za tiba na kwa msingi huo basi ukuangalia hata matokeo ya tiba kwa wanaume ni mabaya kuliko kwa wanawake wote tunajua kwamba kiwango cha maambukizi kipo juu kwa wanawake kuliko wanaume lakini naomba nikwambie kwamba wanaume ndo wanakufa zaidi kwa magonjwa yanayotokana na Ukimwi kuliko wanawake.”

 

“Kama hauendi kwenye huduma na kama hauendi kwenye huduma eitha utapelekwa ukiwa na hali mbaya na matokeo yatakuwa ni mabaya kwaio tafiti zote zinaonyesha hivyo kwa kipindi chote na ndio maana tunaweka msisitizo kwamba sasaivi wanaume tujitokeze tupime ili tujue hali zetu twende tukapate huduma ambazo zinafanana na hali zetu.” amesema Dkt. Kamwera.



Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)