WANANCHI WANGING'OMBE WANOGESHWA MATIBABU BURE YA MACHO

MUUNGANO   MEDIA
0

Wananchi Wilayani Wanging'ombe Mkoani Njombe wamefurahishwa na kupongeza  hatua ya Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Hellen Keller Intl  kwa  kuweza kuwapatia matibabu ya macho bila malipo.


Wananchi hao wametoa pongezi hizo wakati wa zoezi la kambi maalumu ya matibabu ya Macho ikiwemo upasuaji wa mtoto wa jicho inayoendesha na kufadhiliwa na Shirika la Hellen Keller kupitia kampeni ya Cataract kwa kushirikiana na Hospital ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya pamoja na Hospital ya Wilaya ya Wanging'ombe ambapo kupitia kampeni hiyo jumla ya wananchi  900 wenye matatizo mbalimbali ya macho wanatarajiwa kupatiwa huduma mbalimbali ikiwemo dawa na upasuaji huduma hiyo inatolewa na madaktari Bingwa wa Macho kutoka katika Hospital ya Kanda ya Mbeya.






Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)