WAZIRI MCHENGERWA AWAELEKEZA WAKURUGENZI KULIPA FEDHA ZA WATUMISHI WA AJIRA MPYA.

MUUNGANO   MEDIA
0


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed O. Mchengerwa (Mb) amewaelekeza Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanalipa fedha za kujikimu kwa Watumishi wa ajira mpya za Ualimu na Afya walioripoti kwenye vituo vya kazi kuanzia mwezi Julai, 2023. 

Amesema Serikali tayari imeshapeleka fedha kwenye kila Halmashauri kwa ajili ya kulipa stahiki za watumishi hao lakini mpaka leo kuna watumishi wa ajira mpya ambao hawajalipwa fedha za kujikimu, hii sio sawa watumishi wote walipwe fedha za zao kabla ya Oktoba 30, 2023. 


"Fedha za kujikimu ni haki ya kila mwajiriwa mpya sasa, kwanini usilipe na fedha unayo kama kuna changamoto yeyote iwasilishwe ila sio kukaa na fedha na kuacha hawa watumishi wakihangaika, walipwe mara moja." amesisitiza Mhe. Mchengerwa. 


Kwa mwaka wa fedha 2022/23, Serikali iliajiri watumishi wapya wa kada ya Ualimu na Afya ambapo kwa Kada ya Ualimu ni watumishi 13,130 na Afya ni watumishi 7,192 na wote wamekwisharipoti kwenye vituo vyao vya kazi.


Imetolewa na: 

Nteghenjwa Hosseah 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Ofisi ya Rais –TAMISEMI 

03.10.202

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)