MASHINDANO YA SHIMIWI YAPAMBA MOTO IRINGA.

MUUNGANO   MEDIA
0

 


Na. Asila Twaha, Iringa.

Michezo ya SHIMIWI imeendelea kupamba moto katika viwanja mbalimbali Mkoani Iringa ambapo timu mbalimbali zimeendelea kuonyeshana ubabe ambapo timu ya wanawake netiboli TAMISEMI imeipiga  kichapo timu  MASHTAKA  goli 25 -8.


TAMISEMI imeendelea kung'ara baada ya majira ya asubuhi kushinda mchezo wa kuvuta kamba dhidi ya MASHTAKA kwa pointi 2-0


Kichapo  walichozea  timu ya  MASHTAKA kilionekana  katika  dakika 20 za  kwanza ilipofunga goli 13- 2 na hadi mchezo unaisha TAMISEMI ilitoka mbabe kwa goli  25-8.


Kocha wa TAMISEMI Maimuna Kitete amesema bado wanaendelea na mashindano na bado wanaendelea na darasa la kufanya mazoezi  sababu kilichowafanya kushiriki mashindano ya SHIMIWI sio tu kwa kufanya mazoezi ya afya kama watumishi bali pia ni kuhakikisha wanakuwa washindi.

" michezo hujenga afya,umoja,kujuana,kushirikia lakini pia ni ajira" amesema Maimuna


Ametoa wito kwa wachezaji wa timu  kujituma na kuzingatia nidhamu  pindi wanapokuwa  uwanjani na  nje ya uwanja kwa kuwa  kufanya hivyo kutasaidia  kila mchezaji kufikia  lengo lake  la kuwa mchezaji bora.


Kwa upande wa mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji (GA) Flora Odilo amewashukuru viongozi wa Wazira pamoja na watumishi wote kwa kuwatia moyo katika michezo amesema wataendelea kushiriki  na kucheza kwa bidii ili warudi na ushindi.


Naye mchezaji kwa nafasi ya kiungo mchezeshaji senta (C) Lidya Elisha amesema mchezo ni akili  na ushirikiano.






Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)