TIMU YA WANAWAKE YA HAKI SPORTS CLUB YAINYUKA RAS IRINGA MPIRA WA PETE.

MUUNGANO   MEDIA
0

 


Timu ya Wanawake ya Mpira wa Pete ya Haki Sports Club jioni ya leo imeng'ara tena baada ya kujinyakulia ushindi na pointi tatu muhimu dhidi ya timu ya  RAS Iringa.


Akizungumza mara baada ya mchezo huo  Kaptein wa timu hiyo ya Haki Bi. Catherine Saoke amesema kuwa, ushindi huo umepatikana kutokana na kuwa na maandalizi mazuri ya mashindano hayo.

    

Aidha timu hiyo imeendelea kujiweka sawa kwa ajili  ya mchezo wa kesho ambapo kwa upande wa kamba itamenyana na Mawasiliano na upande mpira wa pete itamenyana na MSD.


Kwa upande wa wanaume kesho mapema asubuhi timu ya Haki itamenyana na TARURA.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)