MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA MTINDO WA MAISHA

MUUNGANO   MEDIA
0

 

 

Na.Elimu ya Afya kwa Umma.

Mpendwa msomaji wa safu hii ikiwa tukiwa katika mwezi huu    Julai 14.2023 wa mtindo wa Maisha katika afya(Monthly Healthy Life Styles)  Elimu ya Afya kwa Umma inatumia fursa hii  kukukumbusha kufanya na kuzingatia yafuatayo ili kuendelea kuimarisha afya yako kwani Mtu ni Afya.

      Tumia muda wako kutembea kuliko kuendesha gari(Walk more ,Drive less)

Mara kwa mara  ili kuimarisha afya yako zaidi unashauriwa kutumia muda wako mwingi kutembea kuliko kutumia vyombo vya usafiri kama vile magari, pikipiki,bajaji na vinginevyo vingi kwani hii itasaidia mwili wako kuwa imara na kuepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ,unene kupita kiasi na msukumo wa damu utafanya kazi vizuri, pia utaepuka magonjwa ya moyo na shinikizo la juu la damu.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt.Philip Mpango  katikati akiongoza katika mazoezi ya kutembea moja ya tukio muhimu la bonanza,upande wa kushoto ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na upande wa kulia ni Spika wabunge Dkt.Tulia Ackson .

 


Rais  Mstaafu awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza wapanda mlima Kilimanjaro pamoja na Waendesha baiskeli wanaoshiriki katika  kampeni ya kuchangia fedha za afua ya masuala ya UKIMWI.

     

Ongeza ulaji wa mbogamboga na matunda katika mlo wako(Increase Vegetables and Fruits in your diet).

Mtindo huu wa ulaji wa mbogamboga na matunda unasaidia mwili kupata virutubisho muhimu katika mwili ikiwemo Vitamin C, B6 na K Fat na madini ya shaba na manganese ,kupunguza uwezekano wa magonjwa ya saratani ,Kisukari na maradhi ya moyo ,kuondoa sumu mwilini na kuondoa msongo wa mawazo ,usaidia kupona haraka ukifanyiwa upasuaji hasa ulaji wa tunda la nanasi na matunda mengine mengi.

 


Baadhi ya matunda ambayo ni muhimu kwa ajili ya kujenga afya ya miili yetu.

 Punguza ulaji wa vyakula vyenye mafuta  na  lehemu(Reduce Fats and Cholesterol in your diet ).

Tunaposema lehemu ni mafuta yanayoongezwa mwilini kupitia chakula ,mfano unapokula nyama yale mafuta ya nyama ambayo yana uwezo mkubwa wa kuganda yanaitwa lehemu.

Ikumbukwe kuwa kuna aina mbili za lehemu ambazo ni lehemu nzuri(good  cholesterol) na lehemu mbaya(bad cholesterol),hivyo uwepo wa lehemu mbaya mwilini ndio chanzo kikuu cha uharibifu wa mishipa  ni muhimu kupunguza mtindo wa ulaji wa nyama zenye mafuta mengi hasa nyekundu ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza.

 

     Kunywa maji kwa wingi (Drink more Water).

Kiafya binadamu anashauriwa kunywa maji kwa wingi kwani maji yana faida nyingi ikiwemo kusaidia kuboresha afya ya mfumo wa mkojo hivyo kunywa maji ya kutosha kunasaidia kuondoa hatari ya magonjwa ya Kibofu cha mkojo,maji husaidia kudumisha uzito, kurahisisha mmeng’enyo wa chakula na kuzuia kuvimbiwa,pia maji yana faida kubwa ya kudumisha kumbukumbu na tafiti zinabainisha kuwa mtu akipungukiwa na maji kidogo tu hupoteza kumbukumbu kwa rika lote mtoto au mzee.


Unywaji wa maji ya kutosha ni muhimu katika miili yetu.

 

     Punguza muda wa kutazama runinga na matumizi ya  kompyuta muda mrefu(Reduce your Screen time(TV and Computer).

Katika ulimwengu huu wa utandawazi  matumizi ya runinga na kompyuta yameongezeka maradufu hali ambayo imechagiza watu wengi kutumia muda mwingi kutumia vifaa hivyo vya kielektroniki iwe ofisini au nyumbani licha ya faida yake kuna madhara kiafya  mfano  kuchosha akili na kukosa muda wa kufikiri.


 


     Fanya Mazoezi  ya mwili Mara kwa Mara(Exercise more (body and mind).

Katika mtindo huu wa kufanya mazoezi mara kwa mara inasaidia mwili kuwa imara kwani mtu anayefanya mazoezi  anakuwa na akili inayofikiri na kuchanganua mambo kwa uharaka zaidi, pia mwili wake utakuwa imara katika kukabiliana na magonjwa kama vile maradhi ya moyo .

 




Waziri Mkuu  Mhe. Kassim Majaliwa akiongoza zoezi la kufanya mazezi ya mwili mojawapo ya bonanza la afya  hapa nchini.



Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu akishiriki mazoezi ya viungo na baadhi ya watoto wenye mahitaji maalum katika kuimarisha afya ya mwili.

 

Kula vyakula tofauti tofauti na  vyenye virutubisho vyote muhimu mwilini (Eat a Variety nutritional  of Foods).

Ni muhimu kula vyakula tofauti tofauti na vyenye virutubisho vyote katika mwili kwa kuzingatia makundi yote ikiwemo Protini,Vitamin,Hamirojo kwani hali hiii itasaidia kuujenga vizuri mwili na itakuwa kinga dhidi ya magonjwa .

 

 

Kwa hiyo kupitia mambo yote hayo itatusaidia kuijenga miili yetu kuwa na afya njema  na kuweza kutekeleza majukumu katika ujenzi wa taifa na kila mmoja ana jukumu la kujenga Afya yake kwani  ukiwa na afya dhaifu  huwezi kufanya chochote na jukumu la Elimu ya Afya kwa Umma ni kuelimisha  hivyo sote tujumuike  ili kutimiza adhma ya Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Mpendwa Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri wa Afya  Mhe.Ummy Mwalimu ambapo moja ya vipaumbele ni kuhakikisha afya msingi inakuwa bora kwa kila jamii.

MWISHO.

 

 

 

 

 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)