FAMILIA INAYOKULA MAGUNIA 108

0

 



Halawa Lubana ni  mkulima na mkazi wa Kijiji cha Ikulwe Kata ya Majimoto Halmashauri ya  Mpimbwe Wilayani Mpanda Mkoani Katavi mwenye familia ya watu 26 na mwaka huu amevuna magunia 525 badala ya 700  aliyozoea huku mahitaji ya familia kwa mwaka ni ulaji wa magunia 108  ambapo ametumia fursa hiyo kuwaasa Vijana kuacha kukimbilia mjini bila kazi bali wajikite katika kilimo.

Akizungumza Kijijini hapo Halawa amesema kwa siku familia yake hula debe mbili na mwezi gunia sita hivyo bila jitihada za kulima angeukimbia mji.

“Nawasihi wanaokimbilia mjini bila kazi yoyote waache  kwani ukikimbilia huko mwisho wa siku unakuwa kibaka waje vijijini tulime ,kwa siku natumia debe 2 kwa mwaka magunia 108 bila kukaza buti ningeukimbia mji  na mwaka huu hali siyo nzuri nimepata magunia 525 ya mpunga na mwaka ukiwa mzuri navuna  zaidi ya magunia 700”amesema Lubana.

Katika hatua nyingine Lubana ametoa ushauri kwa serikali kuwasaidia wakulima kupata fursa ya kupima wao wenyenye pindi wanapouza mazao kuliko kupimiwa na wafanyabiashara kwa kutumia ndoo kubwa{rumbesa) huku akitoa shukurani soko la Mpunga kuendelea kuimarika siku hadi siku kwani sasa gunia moja la mpunga wilaya ya Mpanda linauzwa zaidi ya Tsh.laki moja.

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI


Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)