SERIKALI YAISHUKURU KOICA, UBORESHAJI WA MFUMO WA GoTHoMIS MKOA WA DODOMA

0

 









OR- TAMISEMI


Mkurugenzi wa Idara ya  TEHAMA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR-TAMISEMI), Erick Kitali amewashukuru wadau wa maendeleo KOICA na PMC  kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika  kuimarisha usimamizi wa  taarifa za utoaji wa  huduma za afya  kupitia mfumo wa usimamizi wa taarifa za vituo vya afya  (GoT-HoMIS) katika Mkoa wa Dodoma.

 

Kitali amebainisha hayo  Machi 23, 2023 katika kikao kazi cha Kamati ya Ushauri ya mradi wa upanuzi wa matumizi ya mfumo wa 

GoT-HoMIS  katika Mkoa wa Dodoma.


" Tuendelee kushirikiana kwa pamoja kutimiza malengo ya mradi na kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa wananchi" Ameeleza Kitali


Lengo la kikao hiko ni kupitia  na kujadili utekelezaji wa mradi huo  pamoja  na kuweka mipango madhubuti ya utekelezaji wa mradi ili kuongeza wigo  na kuboresha matumizi ya mfumo wa GOT-HOMIS  katika vituo vya kutolea huduma za afya Mkoa wa Dodoma.


Mfumo wa GoT-HoMIS ambao kwa sasa unatumika kwenye vituo zaidi ya 1,400 nchi nzima,  umelenga kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma za afya, kutoa taarifa za magonjwa na wagonjwa kwa usahihi na wakati na kusimamia rasilimali fedha na dawa.  


Kikao  kazi hicho  kimehusisha wataalam kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR-TAMISEMI), Wizara ya Afya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  wadau wa maendeleo KOICA pamoja na PMC.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)